Jina lake halisi anaitwa Nasibu Abdul Juma lakini wengi wanamfahamu kwa jina la Diamond Platnumz, Chibu, Dangote au Simba! Oktoba 2, 1989 ndiyo siku aliyozaliwa! Alizaliwa Tandale, sehemu yenye sifa nyingi za Uswahilini ambazo siyo nzuri sana kuzielezea kwa watu waliomfahamu kupitia mafanikio yake. Ukweli pekee ambao hauwezi kupingika ni kwamba Diamond alizaliwa katika jamii ya watu maskini lakini baadaye akakataa kuishi kinyonge na kuamua kuutumia muziki kama daraja la kumvusha kutoka maisha ya kifukara mpaka kuja kuishi maisha ya kifalme. Safari yake ya muziki, ilianza katikati ya miaka ya 2000 ambapo kwa mara ya kwanza aliingia studio na kurekodi wimbo wa Toka Mwanzo ambao hata hivyo, haukupata mafanikio.
Podchaser is the ultimate destination for podcast data, search, and discovery. Learn More